Wakristo walimtumia Mbunge Wilberforce pamoja na wahubiri kanisani kukaza kampeni kote nchini. Mwaka 1807 walifaulu kupata sheria bungeni iliyopiga marufuku biashara ya watumwa kwa Waingereza na katika makoloni ya Uingereza (lakini watumwa waliokuwepo walibaki hivihivi).